Alhamisi, 9 Julai 2015

Kwetu pazuri yarekodi Santuri muonekano ya 12

Kwaya ya Christian Ambassador kutoka nchini Rwanda wakirekod DVD yao toleo la 12 hivi karibuni (Picha na Warren  na Mutabazi) 

Na Roland Robert

Kundi maarufu la kwaya ya Kisabato kutoka nchini Rwanda, Ambassadors of Christ limerekodi santuri muonekano (DVD) mpya, katika tukio lililofanyika katika viwanja vya chuo kikuu cha Kisabato tawi la Gishushu nchini humo.


Kwamujibu wa blog ya Mtangazaji Maduhu inasema lengo la kurekodi toleo hilo la 12 lenye nyimbo za Kinyarwanda ni kutangaza injili na kuwaunganisha wanyarwanda baada ya mauaji ya kimbali ya mwaka 1994.

Katika rekodi hiyo pia waimbaji waliowahi kuvuma na kwaya hiyo kama solo wao mwanadada Mbabazi Milly Kamugisha alikuwa mmoja wa waimbaji waliorekodi na kwaya yake hiyo baada ya kutubu kisha kurejeshwa kundini miezi kadhaa iliyopita.

Bila kumsahau shemeji na wifi wa Watanzania mwanadada mwenye sauti nzuri ya kwanza aliyeolewa na Mtanzania aitwaye Claire Warren na ambaye makazi yake kwasasa yapo nchini lakini pia alijumuika na wenzake katika tukio hilo 

Ambassadors wakiwa jukwaani tayari kwa zoezi la kurekodi DVD

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni