Hymns

Faith Song Name: Niongoze Safarini: Key E

            Composer:  Elisha Magolana (20011)

1.     Niongoze safrini Bwana unitangulie
      Nisilemewe na dhambi mpaka mwisho wa safari x2
      Duniani kuna giza – Kubwa siwezi kuona
     Jua nalo limekuchwa – Limetoweka na nuru x2

2.     Nimekuchagua wewe kaa ndani yangu mimi
      Na maneno yako Bwana yaniongoze safari x2

           Uniongoze Bwana usinitelekeze
            Neno lako likawe nuru ya miguu yangu
            Daima niwe na wewe Bwana wangu
            Katika mikono yako sitaogopa lolote x2

            Na-a-ku-tegemea Bwana wangu Yesu
            Nimeyakabidhi maisha mikononi mwako
            Hushindwi kitu Bwana, hushindwi jambo lolote
            Sina hofu ninalindwa na jemedari wangu x2

Daima-  Nasonga mbele, nasonga mbele, nasonga mbele,  sitaogopa
Nasema-  Sirudi nyuma, sirudi nyuma, sirudi nyuma maana niko nawe x2


Faith Song Name: Maisha Haya: Key D

            Composer:  Elisha Magolana (20014)

1.   Maisha haya ndugu yangu duniani ni ya muda kitambo tuu- Tunapita
      Hebu safisha njia zako uwe safi siku mauti ikifika wewe- U tayari x2

           Karibu Bwana ingia ndani yangu,
           Safisha sasa maisha yangu eee
           Kwa kuwa mimi sijui siku yangu
           Ya kufa hivyo nitakase Bwana x2

2. Siku za mwanadamu hapa duniani zimejaa shida na taabu-Tunaona
    Tusiwe na huzuni sana yatupasa tumshukuru Mungu yeye-Muumba  wetu x2

          Najua ndugu zangu wataomboleza
          Siku ya kufa kwangu mwenzangu
          Wakizunguka kuaga mwili wangu
          Kama ni safi ni Paradiso tuu x2                

Hei heeee niokoe Bwana aah - usiniache nipotee dhambini
Hei heeee nirehemu Bwana aah- usiniache na mizigo ya dhambi
Yahweee nisafishe Bwana aah- usiniache na uovu wangu
Yahweee niongoze Bwana aah- usiniache kati ya maadui x2 

Faith Song Name: Bwana Ulinichagua: Key D

            Composer:  Elisha Magolana (20014)

     1. Bwana ulinichagua mimi, ili- nikutumi-kie wewe
         Nakumbuka nyakati zile, nakumbuka pendo lako
         Nili-asi wi-to wako Bwana, Kwa ku-penda mambo ya dunia
         Najutia zamani zile, najutia uamuzi wangu x2

  Ee Bwana Yesu narudi nipokee mwanao
  Dunia imenisonga sina pa kutokea x2
  Wewe msaada wangu, tena kimbilio langu x2

  Utukuzwe Mungu juu mbinguni, usifiwe kwa upendo wako x2    
  Wewe ndiwe dhamana ya maisha yangu naja kwako kwa uzuri Bwana aaah                    Umenipa urithi kwa waokovu wako, naahidi kuwa nawe Bwana aaah x2

Bwana Mungu hapendezwi kuwaona wanadamu wakipote
Kamtuma Yesu Kristo kuja hapa dunia kutuokoax2

 Jipeleleze, Matendo yako.........Oooh   
 Mwenendo wako, Maisha yako x2

Faith Song Name: Tembea na Yesu: Key D

            Composer:  Elisha Magolana (20014)

Ulimwenguni tunayo vita kuubwa na ya kutisha mwovu shetani ameivuruga dunia,
Si kwa watoto, si kwa vijana hata watu wazima Ibirisi amewachakaza kabisa x2.

Dunia ni shida inanuka dhambi  sasa Aah, hata utu wetu umezidiwa na wanyama,
Yasikitisha sana ndoa za jinsia moja Aah, zinaingia makanisani kubarikiwa x2 

Mwenzangu amani ya kweli yapatikana yapatikana kwa Yesu
Mwenzangu furaha ya kweli yapatikana yapatikana kwa Yesu x2  

             Oh! Tembea ah - Na Yesu
             Safiri  -  Na Yesu
             Kazini - Na Yesu,        
             Sokoni - Na Yesu  x2

             Popote tembea na Yesu, siku zote tembea na Yesu
             Masomoni tembea na Yesu, usimwache tembea na Yesu x2

Rafiki yangu mmoja wa karibu Eeeh alipotajirika akamwacha Yesu
Nilipomuuliza alijibu Eeeh kwamba huko kwa Yesu hakuna starehe x2
Laiti angejua kwa Yesu kwa Yesu iko furaha ya milele x2.

           Oo! Tenda Bwana - Tenda kitu
           Kwa makutano - Tenda kitu
           Ili watu -wakuone wewe - Tenda Bwana x2 

Faith Song Name: Nimekukimbilia wewe: Key F

            Composer:  Elisha Magolana (20015)


Nimekukimbilia wewe- Mungu wangu okoa maisha yangu naye mwovu.
Nimekutumaini wewe- Nisi-aibike adui wasifurahi kunisinda x 2

          Nakimbilia kwako Ee baba
          Niepushe na mabaya ya dunia
          Bila masaada wako nitashindwa
          Baba ninakuomba uniponye x2

Chunga sasa maisha yangu- Niokoe wateesi wanifuata uniponye.
Uniongoze katika haki- Nifundishe mapito yako baba unirehemu x2

Inapendeza ndugu yangu,  kumpokea huyu Yesu
Ayatawale maisha yako, Atasamehe dhambi zako x2 


Faith Song Name: Wavuvi: Key D

Composer:  Elisha Magolana (20015)

Bwana Yesu alikuwa akipita kando
Kando ya ziwa Galilaya akihubiri
Akawaona wavuvi Simoni na Andrea
Wakivua samaki kwa nyavu zao x2.

          Ndipo Yesu akawaambia,  nifuateni mimi nitawabadilisha
          Nanyi mtakuwa wavuvi wa watu, na kuware-je-sha wale                   waliopotea x2.

           Wakaondoka kumfuata Bwana Yesu
           Waliziacha nyavu zao kwa haraka
           Fundisho kwetu tusikiapo sauti
           Tumfuate Yesu na kuacha dhambi zetu x2

Ni Yesu pekee anaweza kukusamehe - Na kukubadilisha
Ni Yesu pekee ndiye jibu la matatizo -Hebu mwite leo.... yako x2 

Song Name : Ebenezer 

By Angela Chibalonza

Umbali tumetoka, na mahali tumefika (This far we have come from, and where we are now)
Ndio maana ninatambua, kwamba wewe ni ebeneza (It is why I confess, that you are Ebenezer)
Sio kwa uwezo wangu,ila ni kwa uwezo wako (It is not because of my might, but by yours)
Mahali nimefika, acha nikushukuru (Thus far I have reached, let me thank you)
EE Bwana umenisaidia, nifike mahali nimefika (Oh Lord you have helped me, to reach where I am)
Bwana wewe ni ebeneza, maishani mwangu oo (Lord you are the Ebenezer in my life)

Ninataka Ebeneza, nijenge juu yako (I want to build on you Ebenezer)
Ninataka Ebeneza, uwe msingi yangu (I want you Ebenezer to be my foundation)
Jiwe langu la pembeni, nakutamani sana (My cornerstone, I desire you so much)
Jiwe langu la thamani, nakuhitaji sana (My valuable rock, I need you so much)
Oo Ebeneza, jiwe langu (Oh Ebenezer, my rock)

Ninataka maisha yangu, yajengwe juu yako (I want my life, to be founded on you)
NInataka ndoa yangu, ijengwe juu yako baba (I want my marriage, to be founded on you)
Ndoa zilizojengwa juu yako yahwe, hazivunjiki kamwe (because marriages built on you, can never be broken)
Nyumba zilizojengwa juu yako yahweh hazivunjiki kamwe (Homes founded on you Yahweh, can never be broken)
Ninataka uimbaji wangu baba, ujengwe juu yako (I want my singing Father, to be founded on you)
Maana wewe ni sauti yangu, wewe ni uzima wangu (For you are my voice, you are my life)

Ninataka Ebeneza, nijenge juu yako (I want to build on you Ebenezer)
Ninataka Ebeneza, uwe msingi yangu (I want you Ebenezer to be my foundation)
Jiwe langu la pembeni, nakutamani sana (My cornerstone, I desire you so much)
Jiwe langu la thamani, nakuhitaji sana (My valuable rock, I need you so much)
Oo Ebeneza, jiwe langu (Oh Ebenezer, my rock)

Ebeneza lang’a, libanga nangai ya tala
Ole kidya mape wolo papa ee kati na bomoyi nanga
Nzambe na kumisio, mokote ko nani nayo
Bisika nako milele o yahwe, ezali sela makasi nayo

Ninataka Ebeneza, nijenge juu yako (I want to build on you Ebenezer)
Ninataka Ebeneza, uwe msingi yangu (I want you Ebenezer to be my foundation)
Jiwe langu la pembeni, nakutamani sana (My cornerstone, I desire you so much)
Jiwe langu la thamani, nakuhitaji sana (My valuable rock, I need you so much)
Oo Ebeneza, jiwe langu (Oh Ebenezer, my rock)

Ebenezer ni jiwe langu, jiwe langu la msingi (Ebenezer is my rock, my cornerstone)
Mahali nimefika leo, Ni kwa ajili yako ebeneza (Thus far I have come, is because of you Ebenezer)
Mawe mengi yako hapa chini ya jua (There are a lot of rocks under the sun)
kuna dhahabu, kuna almasi Kuna mawe hata sijui majina yake (There is gold, there is diamond, and others I can’t name)
Lakini hakutawahi kuwa jiwe kama ebeneza (But there will never be a rock like Ebenezer)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni